‏ Psalms 96

Mungu Mfalme Mkuu

(1 Nyakati 16:23-33)

1 aMwimbieni Bwana wimbo mpya;
mwimbieni Bwana dunia yote.
2 bMwimbieni Bwana, lisifuni jina lake;
tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
3 cTangazeni utukufu wake katikati ya mataifa,
matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.

4 dKwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote;
yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
5 eKwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu,
lakini Bwana aliziumba mbingu.
6 fFahari na enzi viko mbele yake;
nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.

7 gMpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa,
mpeni Bwana utukufu na nguvu.
8 hMpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake;
leteni sadaka na mje katika nyua zake.
9 iMwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake;
dunia yote na itetemeke mbele zake.

10 jKatikati ya mataifa semeni, “Bwana anatawala.”
Ulimwengu ameuweka imara, hauwezi kusogezwa;
atawahukumu watu kwa uadilifu.
11 kMbingu na zishangilie, nchi na ifurahi;
bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake;
12 lmashamba na yashangilie,
pamoja na vyote vilivyomo ndani yake.
Kisha miti yote ya msituni itaimba kwa furaha;
13 mitaimba mbele za Bwana kwa maana anakuja,
anakuja kuihukumu dunia.
Ataihukumu dunia kwa haki,
na mataifa katika kweli yake.
Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.

Everyone uses cookies. We do too! Cookies are little bits of information stored on your computer which help us give you a better experience. You can find out more by reading the STEPBible cookie policy.