‏ Psalms 51:1-9

Kuomba Msamaha

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Baada ya kukemewa na nabii Nathani kwa kuzini na Bathsheba.

1 aEe Mungu, unihurumie,
kwa kadiri ya upendo wako usiokoma,
kwa kadiri ya huruma yako kuu,
uyafute makosa yangu.
2 bUnioshe na uovu wangu wote
na unitakase dhambi yangu.

3 cKwa maana ninajua makosa yangu,
na dhambi yangu iko mbele yangu daima.
4 dDhidi yako, wewe peke yako, nimetenda dhambi
na kufanya yaliyo mabaya machoni pako,
ili uthibitike kuwa wa kweli unenapo,
na kuwa na haki utoapo hukumu.
5 eHakika mimi nilizaliwa mwenye dhambi,
mwenye dhambi tangu nilipotungwa mimba kwa mama yangu.
6 fHakika wewe wapendezwa na kweli itokayo moyoni,
ndani sana ya moyo wangu wanifundisha hekima.

7 gNioshe kwa hisopo, nami nitakuwa safi,
unisafishe, nami nitakuwa mweupe kuliko theluji.
8 hUnipe kusikia furaha na shangwe,
mifupa uliyoiponda na ifurahi.
9 iUfiche uso wako usizitazame dhambi zangu,
na uufute uovu wangu wote.

Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.