‏ Psalms 20:1-4

Maombi Kwa Ajili Ya Ushindi

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.

1 a Bwana na akujibu unapokuwa katika dhiki,
jina la Mungu wa Yakobo na liwe kinga yako.
2 bNa akutumie msaada kutoka patakatifu
na akupatie msaada kutoka Sayuni.
3 cNa azikumbuke dhabihu zako zote,
na azikubali sadaka zako za kuteketezwa.
4 dNa akujalie haja ya moyo wako,
na aifanikishe mipango yako yote.

Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.