‏ Psalms 2:1-5

Mfalme Aliyechaguliwa Na Mungu

1 aKwa nini mataifa wanashauriana kufanya mabaya,
na kabila za watu kula njama bure?
2 b cWafalme wa dunia wanajipanga
na watawala wanajikusanya pamoja
dhidi ya Bwana
na dhidi ya Mpakwa Mafuta wake.
3 dWanasema, “Tuvunje minyororo yao
na kuvitupilia mbali vifungo vyao.”

4 eYeye atawalaye mbinguni hucheka,
Bwana huwadharau.
5 fKisha huwakemea katika hasira yake
na kuwaogopesha katika ghadhabu yake, akisema,

Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.