‏ Psalms 132:1-5

Maskani Ya Mungu Ya Milele Katika Sayuni

Wimbo wa kwenda juu.

1Ee Bwana, mkumbuke Daudi
na taabu zote alizozistahimili.

2 aAliapa kiapo kwa Bwana
na akaweka nadhiri kwa Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo:
3 b“Sitaingia nyumbani mwangu
au kwenda kitandani mwangu:
4 csitaruhusu usingizi katika macho yangu,
wala kope zangu kusinzia,
5 dmpaka nitakapompatia Bwana mahali,
makao kwa ajili ya Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo.”
Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.