‏ Psalms 112:2-9


2 aWatoto wake watakuwa wenye uwezo katika nchi,
kizazi cha watu waadilifu kitabarikiwa.
3 bNyumbani mwake kuna mali na utajiri,
haki yake hudumu milele.
4 cHata gizani nuru humzukia mtu mwadilifu,
yule mwenye rehema, huruma na haki.

5 dMema yatamjia mtu yule aliye mkarimu na mwenye kukopesha bila riba,
anayefanya mambo yake kwa haki.
6 eHakika hatatikisika kamwe,
mtu mwenye haki atakumbukwa milele.
7 fHataogopa habari mbaya,
moyo wake ni thabiti, ukimtegemea Bwana.
8 gMoyo wake ni salama, hatakuwa na hofu,
mwishoni ataona ushindi dhidi ya adui zake.
9 hAmetawanya vipawa vyake kwa ukarimu akawapa maskini;
haki yake hudumu milele;
pembe yake itatukuzwa kwa heshima.
Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.