‏ Proverbs 2:6-10

6 aKwa maana Bwana hutoa hekima,
na kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu.
7 bAnahifadhi ushindi kwa ajili ya mwadilifu,
yeye ni ngao kwa wale wasio na lawama,
8 ckwa kuwa hulinda mwenendo wa mwenye haki
na kuhifadhi njia ya waaminifu wake.

9 dNdipo utafahamu lipi lililo kweli na haki
na sawa: yaani kila njia nzuri.
10 eKwa maana hekima itaingia moyoni mwako,
nayo maarifa yataifurahisha nafsi yako.

Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.