‏ Proverbs 2:1-9

Faida Za Hekima

1 aMwanangu, kama utayakubali maneno yangu
na kuyaweka akiba maagizo yangu ndani mwako,
2 bkutega sikio lako kwenye hekima
na kuweka moyo wako katika ufahamu,
3 cna kama ukiita busara
na kuita kwa sauti ufahamu,
4 dna kama utaitafuta kama fedha
na kuitafuta sana kama hazina iliyofichwa,
5 endipo utakapoelewa kumcha Bwana
na kupata maarifa ya Mungu.
6 fKwa maana Bwana hutoa hekima,
na kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu.
7 gAnahifadhi ushindi kwa ajili ya mwadilifu,
yeye ni ngao kwa wale wasio na lawama,
8 hkwa kuwa hulinda mwenendo wa mwenye haki
na kuhifadhi njia ya waaminifu wake.

9 iNdipo utafahamu lipi lililo kweli na haki
na sawa: yaani kila njia nzuri.

Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.