‏ Numbers 14:1-4

Watu Wanaasi

1 aUsiku ule watu wote wa jumuiya walipaza sauti zao na kulia kwa sauti kuu. 2 bWaisraeli wote wakanungʼunika dhidi ya Mose na Aroni, nalo kusanyiko lote wakawaambia, “Laiti tungekuwa tumefia humo nchi ya Misri! Au humu kwenye hili jangwa! 3 cKwa nini Bwana anatuleta katika nchi hii ili tufe kwa upanga? Wake zetu na watoto wetu watachukuliwa kama nyara. Je, isingekuwa bora kwetu kurudi Misri?” 4 dWakasemezana wao kwa wao, “Inatupasa kumchagua kiongozi na kurudi Misri.”

Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.