‏ Job 3:16-22

16 aAu kwa nini sikufichwa ardhini kama mtoto aliyezaliwa mfu,
kama mtoto mchanga ambaye kamwe hakuuona mwanga?
17 bHuko waovu huacha kusumbua
na huko waliochoka hupumzika.
18 cWafungwa nao hufurahia utulivu wao,
hawasikii tena sauti ya kukemea ya kiongozi wa watumwa.
19 dWadogo na wakubwa wamo humo,
na mtumwa ameachiwa huru kutoka kwa bwana wake.

20 e“Mbona nuru inawaangazia wale walio taabuni,
na hao wenye uchungu kupewa uhai,
21 fwale wanaotamani kifo ambacho hakiji,
wale watafutao kufa zaidi ya kutafuta hazina iliyofichwa,
22 gambao hujawa na furaha,
na hushangilia wafikapo kaburini?

Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.