‏ Isaiah 17:1-3

Neno Dhidi Ya Dameski

1 aNeno kuhusu Dameski:

“Tazama, Dameski haitakuwa tena mji
bali itakuwa lundo la magofu.
2 bMiji ya Aroeri itaachwa
na itaachiwa mifugo ambayo italala huko,
bila yeyote wa kuyaogopesha.
3 cMji wenye ngome utatoweka kutoka Efraimu,
nao uweza wa ufalme kutoka Dameski;
mabaki ya Aramu yatakuwa
kama utukufu wa Waisraeli,”
asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.

Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.