‏ Ephesians 4:7-10

7 aLakini kila mmoja wetu amepewa neema kwa kadiri ya kipimo cha kipawa cha Kristo. 8 bKwa hiyo husema:

“Alipopaa juu zaidi,
Juu zaidi hapa ina maana mbingu za mbingu.

aliteka mateka,
akawapa wanadamu vipawa.”
9 d(Asemapo “alipaa juu,” maana yake nini isipokuwa ni kusema pia kwamba Kristo alishuka pande za chini sana za dunia?
Pande za chini sana za dunia hapa maana yake Sheol kwa Kiebrania, yaani Kuzimu.
10 fYeye aliyeshuka ndiye alipaa juu zaidi kupita mbingu zote, ili apate kuujaza ulimwengu wote.)
Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.

Everyone uses cookies. We do too! Cookies are little bits of information stored on your computer which help us give you a better experience. You can find out more by reading the STEPBible cookie policy.