‏ Deuteronomy 6:4-9

4 aSikia, ee Israeli: Bwana Mungu wako, Bwana ni mmoja. 5 bMpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote. 6 cAmri hizi ninazokupa leo zitakuwa katika moyo wako. 7 dWafundishe watoto wako kwa bidii. Nena kuhusu amri hizi uketipo nyumbani na wakati utembeapo njiani, ulalapo na uamkapo. 8 eZifunge kama alama juu ya mkono wako, na uzifunge juu ya paji la uso wako. 9 fZiandike kwenye miimo ya milango ya nyumba yako na juu ya malango yako.


Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.