‏ Psalms 87

Sifa Za Yerusalemu

Zaburi ya wana wa Kora. Wimbo.

1 aAmeuweka msingi wake katika mlima mtakatifu;
2 b Bwana anayapenda malango ya Sayuni
kuliko makao yote ya Yakobo.
3 cMambo matukufu yanasemwa juu yako,
ee mji wa Mungu:
4 d“Nitaweka kumbukumbu ya Rahabu
Rahabu hapa ni jina la ushairi la Misri.
na Babeli
miongoni mwa wale wanaonikubali mimi:
Ufilisti pia na Tiro, pamoja na Kushi,
Kushi hapa ina maana ya Naili ya juu, yaani Ethiopia.

nami nitasema, ‘Huyu alizaliwa Sayuni.’ ”

5 gKuhusu Sayuni itasemwa hivi,
“Huyu na yule walizaliwa humo,
naye Aliye Juu Sana mwenyewe
atamwimarisha.”
6 h Bwana ataandika katika orodha ya mataifa:
“Huyu alizaliwa Sayuni.”
7 iWatakapokuwa wanapiga vinanda wataimba,
“Chemchemi zangu zote ziko kwako.”
Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.

Everyone uses cookies. We do too! Cookies are little bits of information stored on your computer which help us give you a better experience. You can find out more by reading the STEPBible cookie policy.