‏ Psalms 6

Sala Kwa Ajili Ya Msaada Wakati Wa Taabu

Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Mtindo wa sheminithi.
Sheminithi ni mtajo mmojawapo katika lugha ya uimbaji.
Zaburi ya Daudi.

1 bEe Bwana, usinikemee katika hasira yako,
wala usiniadhibu katika ghadhabu yako.
2 cUnirehemu Bwana,
kwa maana nimedhoofika;
Ee Bwana, uniponye,
kwa maana mifupa yangu
ina maumivu makali.
3 dNafsi yangu ina uchungu mwingi.
Mpaka lini, Ee Bwana, mpaka lini?

4 eGeuka Ee Bwana, unikomboe,
uniokoe kwa sababu ya fadhili zako.
5 fHakuna mtu anayekukumbuka
akiwa amekufa.
Ni nani awezaye kukusifu
akiwa kuzimu?

6 gNimechakaa kwa kulia kwa huzuni;
usiku kucha nafurikisha
kitanda changu kwa machozi;
nimelowesha viti vyangu vya fahari
kwa machozi.
7 hMacho yangu yamedhoofika kwa kuhuzunika,
yamedhoofika kwa sababu ya adui zangu wote.

8 iKaeni mbali nami, ninyi nyote mtendao mabaya,
kwa maana Bwana amesikia kulia kwangu.
9 j Bwana amesikia kilio changu kwa huruma,
Bwana amekubali sala yangu.
10 kAdui zangu wote wataaibika na kufadhaika,
watarudi nyuma kwa aibu ya ghafula.
Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.