‏ Psalms 46

Mungu Yuko Pamoja Nasi

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya wana wa Kora. Mtindo wa alamothi.

1 aMungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu,
msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso.
2 bKwa hiyo hatutaogopa, hata kama dunia ikiondolewa
nayo milima ikiangukia moyoni mwa bahari.
3 cHata kama maji yake yatanguruma na kuumuka,
milima nayo ikitetemeka kwa mawimbi yake.

4 dKuna mto ambao vijito vyake vinaufurahisha mji wa Mungu,
mahali patakatifu ambako Aliye Juu Sana anaishi.
5 eMungu yuko katikati yake, hautaanguka,
Mungu atausaidia asubuhi na mapema.
6 fMataifa yanafanya ghasia, falme zinaanguka,
Yeye huinua sauti yake, dunia ikayeyuka.

7 g Bwana Mwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi,
Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.

8 hNjooni mkaone kazi za Bwana
jinsi alivyofanya ukiwa katika nchi.
9 iAnakomesha vita hata miisho ya dunia,
anakata upinde na kuvunjavunja mkuki,
anateketeza ngao kwa moto.
10 j“Tulieni, mjue ya kwamba mimi ndimi Mungu;
nitatukuzwa katikati ya mataifa,
nitatukuzwa katika dunia.”

11 Bwana Mwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi;
Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.
Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.