‏ Psalms 29

Sauti Ya Bwana Wakati Wa Dhoruba

Zaburi ya Daudi.

1 aMpeni Bwana, enyi mashujaa,
mpeni Bwana utukufu na nguvu.
2 bMpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake;
mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake.
3 cSauti ya Bwana iko juu ya maji;
Mungu wa utukufu hupiga radi,
Bwana hupiga radi juu ya maji makuu.

4 dSauti ya Bwana ina nguvu;
sauti ya Bwana ni tukufu.
5 eSauti ya Bwana huvunja mierezi;
Bwana huvunja vipande vipande
mierezi ya Lebanoni.
6 fHufanya Lebanoni irukaruke kama ndama,
Sirioni
Yaani Mlima Hermoni.
urukaruke kama mwana nyati.
7 hSauti ya Bwana hupiga kwa miali
ya umeme wa radi.
8 iSauti ya Bwana hutikisa jangwa;
Bwana hutikisa Jangwa la Kadeshi.
9 jSauti ya Bwana huzalisha ayala,
na huuacha msitu wazi.
Hekaluni mwake wote wasema,
“Utukufu!”

10 k Bwana huketi akiwa ametawazwa juu ya gharika;
Bwana ametawazwa kuwa Mfalme milele.
11 l Bwana huwapa watu wake nguvu;
Bwana huwabariki watu wake kwa kuwapa amani.
Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.