‏ Psalms 28

Kuomba Msaada

Zaburi ya Daudi.

1 aNinakuita wewe, Ee Bwana, Mwamba wangu;
usiwe kwangu kama kiziwi.
Kwa sababu ukinyamaza
nitafanana na walioshuka shimoni.
2 bSikia kilio changu unihurumie
ninapokuita kwa ajili ya msaada,
niinuapo mikono yangu kuelekea
Patakatifu pa Patakatifu pako.

3 cUsiniburute pamoja na waovu,
pamoja na hao watendao mabaya,
ambao huzungumza na jirani zao maneno mazuri,
lakini mioyoni mwao wameficha chuki.
4 dWalipe sawasawa na matendo yao,
sawasawa na matendo yao maovu;
walipe sawasawa na kazi za mikono yao,
uwalipe wanavyostahili.
5 eKwa kuwa hawaheshimu kazi za Bwana,
na yale ambayo mikono yake imetenda,
atawabomoa na kamwe
hatawajenga tena.

6 f Bwana asifiwe,
kwa maana amesikia kilio changu
nikimwomba anihurumie.
7 g Bwana ni nguvu zangu na ngao yangu,
moyo wangu umemtumaini yeye,
nami nimesaidiwa.
Moyo wangu unarukaruka kwa furaha
nami nitamshukuru kwa wimbo.

8 h Bwana ni nguvu ya watu wake,
ngome ya wokovu kwa mpakwa mafuta wake.
9 iWaokoe watu wako na uubariki urithi wako;
uwe mchungaji wao na uwabebe milele.
Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.

Everyone uses cookies. We do too! Cookies are little bits of information stored on your computer which help us give you a better experience. You can find out more by reading the STEPBible cookie policy.