‏ Psalms 20

Maombi Kwa Ajili Ya Ushindi

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.

1 a Bwana na akujibu unapokuwa katika dhiki,
jina la Mungu wa Yakobo na liwe kinga yako.
2 bNa akutumie msaada kutoka patakatifu
na akupatie msaada kutoka Sayuni.
3 cNa azikumbuke dhabihu zako zote,
na azikubali sadaka zako za kuteketezwa.
4 dNa akujalie haja ya moyo wako,
na aifanikishe mipango yako yote.
5 eTutashangilia kwa furaha utakaposhinda,
tutainua bendera zetu kwa jina la Mungu wetu.
Bwana na akupe haja zako zote.

6 fSasa nafahamu kuwa Bwana
humwokoa mpakwa mafuta wake,
humjibu kutoka mbingu yake takatifu
kwa nguvu za wokovu wa mkono wake wa kuume.
7 gWengine wanatumaini magari ya vita, na wengine farasi,
bali sisi tutalitumainia jina la Bwana, Mungu wetu.
8 hWao wameshushwa chini na kuanguka,
bali sisi tunainuka na kusimama imara.

9 iEe Bwana, mwokoe mfalme!
Tujibu tunapokuita!
Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.