‏ Psalms 13

Sala Ya Kuomba Msaada

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.

1 a bMpaka lini, Ee Bwana? Je, utanisahau milele?
Utanificha uso wako mpaka lini?
2 cNitapambana na mawazo yangu mpaka lini,
na kila siku kuwa na majonzi moyoni mwangu?
Adui zangu watanishinda mpaka lini?

3 dNitazame, unijibu, Ee Bwana Mungu wangu.
Yatie nuru macho yangu,
ama sivyo nitalala usingizi wa mauti.
4 eAdui yangu atasema, “Nimemshinda,”
nao adui zangu watashangilia nitakapoanguka.

5 fLakini ninategemea upendo wako usiokoma;
moyo wangu unashangilia katika wokovu wako.
6 gNitamwimbia Bwana,
kwa kuwa amekuwa mwema kwangu.
Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.