‏ Psalms 12

Kuomba Msaada

Kwa mwimbishaji. Mtindo wa sheminithi. Zaburi ya Daudi.

1 a Bwana tusaidie, kwa kuwa wacha Mungu wametoweka;
waaminifu wametoweka miongoni mwa wanadamu.
2 bKila mmoja humwambia jirani yake uongo;
midomo yao ya hila huzungumza kwa udanganyifu.

3 c Bwana na akatilie mbali midomo yote ya hila
na kila ulimi uliojaa majivuno,
4 dule unaosema, “Kwa ndimi zetu tutashinda;
midomo ni mali yetu, bwana wetu ni nani?”

5 e“Kwa sababu ya uonevu wa wanyonge
na kulia kwa uchungu kwa wahitaji,
nitainuka sasa,” asema Bwana.
“Nitawalinda kutokana na wale
wenye nia mbaya juu yao.”
6 fManeno ya Bwana ni safi,
kama fedha iliyosafishwa katika tanuru,
iliyosafishwa mara saba.

7 gEe Bwana, utatuweka salama
na kutulinda na kizazi hiki milele.
8 hWatu waovu huenda wakiringa kila mahali
wakati ambapo yule aliye mbaya sana
ndiye anayeheshimiwa miongoni mwa watu.
Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.