‏ Psalms 149

Wimbo Wa Kumsifu Mungu Kwa Wema Wake

1 aMsifuni Bwana.

Mwimbieni Bwana wimbo mpya,
sifa zake katika kusanyiko la watakatifu.

2 bIsraeli na washangilie katika Muumba wao,
watu wa Sayuni na wafurahi katika Mfalme wao.
3 cNa walisifu jina lake kwa kucheza
na wampigie muziki kwa matari na kinubi.
4 dKwa maana Bwana anapendezwa na watu wake,
anawavika wanyenyekevu taji ya wokovu.
5 eWatakatifu washangilie katika heshima hii,
na waimbe kwa shangwe vitandani mwao.

6 fSifa za Mungu na ziwe vinywani mwao
na upanga ukatao kuwili mikononi mwao,
7 gili walipize mataifa kisasi
na adhabu juu ya mataifa,
8 hwawafunge wafalme wao kwa minyororo,
wakuu wao kwa pingu za chuma,
9 iili kuwafanyia hukumu iliyoandikwa dhidi yao.
Huu ndio utukufu wa watakatifu wake wote.

Msifuni Bwana.
Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.

Everyone uses cookies. We do too! Cookies are little bits of information stored on your computer which help us give you a better experience. You can find out more by reading the STEPBible cookie policy.