‏ Psalms 138

Maombi Ya Shukrani

Zaburi ya Daudi.

1 aNitakusifu wewe, Ee Bwana, kwa moyo wangu wote,
mbele ya “miungu” nitaimba sifa zako.
2 bNitasujudu nikielekea Hekalu lako takatifu,
nami nitalisifu jina lako
kwa ajili ya upendo wako
na uaminifu,
kwa kuwa umelikuza jina lako na neno lako
juu ya vitu vyote.
3 cNilipoita, ulinijibu;
ulinifanya jasiri na mwenye moyo hodari.

4 dWafalme wote wa dunia wakusifu wewe Ee Bwana,
wakati wanaposikia maneno ya kinywa chako.
5 eWao na waimbe kuhusu njia za Bwana,
kwa maana utukufu wa Bwana ni mkuu.

6 fIngawa Bwana yuko juu,
humwangalia mnyonge,
bali mwenye kiburi
yeye anamjua kutokea mbali.
7 gNijapopita katikati ya shida,
wewe unayahifadhi maisha yangu,
unanyoosha mkono wako dhidi ya hasira ya adui zangu,
kwa mkono wako wa kuume unaniokoa.
8 h Bwana atatimiza kusudi lake kwangu,
Ee Bwana, upendo wako wadumu milele:
usiziache kazi za mikono yako.
Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.