‏ Psalms 129

Maombi Dhidi Ya Adui Za Israeli

Wimbo wa kwenda juu.

1 aWamenionea mno tangu ujana wangu;
Israeli na aseme sasa:
2 bwamenionea mno tangu ujana wangu,
lakini bado hawajanishinda.
3 cWakulima wamelima mgongo wangu,
na kufanya mifereji yao mirefu.
4 dLakini Bwana ni mwenye haki;
amenifungua toka kamba za waovu.

5 eWale wote waichukiao Sayuni
na warudishwe nyuma kwa aibu.
6 fWawe kama majani juu ya paa,
ambayo hunyauka kabla hayajakua;
7 gkwa hayo mvunaji hawezi kujaza vitanga vyake,
wala akusanyaye kujaza mikono yake.
8 hWale wapitao karibu na wasiseme,
“Baraka ya Bwana iwe juu yako;
tunakubariki katika jina la Bwana.”
Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.

Everyone uses cookies. We do too! Cookies are little bits of information stored on your computer which help us give you a better experience. You can find out more by reading the STEPBible cookie policy.