‏ Psalms 126

Kurejezwa Kutoka Utumwani

Wimbo wa kwenda juu.

1 a Bwana alipowarejeza mateka Sayuni,
tulikuwa kama watu walioota ndoto.
2 bVinywa vyetu vilijaa kicheko,
ndimi zetu zilijaa nyimbo za shangwe.
Ndipo iliposemwa miongoni mwa mataifa,
Bwana amewatendea mambo makuu.”
3 c Bwana ametutendea mambo makuu,
nasi tumejaa furaha.

4 dEe Bwana, turejeshee watu wetu waliotekwa,
kama vijito katika Negebu.
5 eWapandao kwa machozi
watavuna kwa nyimbo za shangwe.
6Yeye azichukuaye mbegu zake
kwenda kupanda, huku akilia,
atarudi kwa nyimbo za shangwe,
akichukua miganda ya mavuno yake.
Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.