‏ Psalms 124

Shukrani Kwa Ukombozi Wa Israeli

Wimbo wa kwenda juu. Wa Daudi.

1 aKama Bwana asingalikuwa upande wetu;
Israeli na aseme sasa:
2kama Bwana asingalikuwa upande wetu,
wakati watu walipotushambulia,
3 bwakati hasira yao ilipowaka dhidi yetu,
wangalitumeza tungali hai,
4 cmafuriko yangalitugharikisha,
maji mengi yangalitufunika,
5maji yaendayo kasi
yangalituchukua.

6 Bwana asifiwe,
yeye ambaye hakuruhusu turaruliwe kwa meno yao.
7 dTumeponyoka kama ndege
kutoka mtego wa mwindaji;
mtego umevunjika,
nasi tukaokoka.
8 eMsaada wetu ni katika jina la Bwana,
Muumba wa mbingu na dunia.
Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.