‏ Psalms 122

Sifa Kwa Yerusalemu

Wimbo wa kwenda juu. Wa Daudi.

1 aNilishangilia pamoja na wale walioniambia,
“Twende nyumbani ya Bwana.”
2Ee Yerusalemu, miguu yetu imesimama
malangoni mwako.

3 bYerusalemu imejengwa vyema kama mji
ambao umeshikamanishwa pamoja.
4 cHuko ndiko makabila hukwea,
makabila ya Bwana,
kulisifu jina la Bwana kulingana na maagizo
waliopewa Israeli.
5Huko viti vya enzi vya hukumu hukaa,
viti vya enzi vya nyumba ya Daudi.

6 dOmba kwa ajili ya amani ya Yerusalemu:
“Wote wakupendao na wawe salama.
7 eAmani na iwepo ndani ya kuta zako
na usalama ndani ya ngome zako.”
8Kwa ajili ya ndugu zangu na marafiki,
nitasema, “Amani iwe ndani yako.”
9 fKwa ajili ya nyumba ya Bwana Mungu wetu,
nitatafuta mafanikio yako.
Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.