‏ Psalms 121

Bwana Mlinzi Wetu

Wimbo wa kwenda juu.

1Nayainua macho yangu nitazame vilima,
msaada wangu utatoka wapi?
2 aMsaada wangu hutoka kwa Bwana,
Muumba wa mbingu na dunia.

3 bHatauacha mguu wako uteleze,
yeye akulindaye hatasinzia,
4 chakika, yeye alindaye Israeli
hatasinzia wala hatalala usingizi.
5 d Bwana anakulinda,
Bwana ni uvuli wako mkono wako wa kuume,
6 ejua halitakudhuru mchana,
wala mwezi wakati wa usiku.
7 f Bwana atakukinga na madhara yote,
atayalinda maisha yako,
8 g Bwana atakulinda unapoingia na unapotoka,
tangu sasa na hata milele.
Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.