‏ Psalms 114

Maajabu Ya Mungu Wakati Israeli Walipotoka Misri

1 aWakati Israeli walipotoka Misri,
nyumba ya Yakobo kutoka kwa watu wa lugha ngeni,
2 bYuda alifanywa makao matakatifu ya Mungu,
Israeli akawa milki yake.

3 cBahari ilitazama ikakimbia,
Yordani ulirudi nyuma,
4 dmilima ilirukaruka kama kondoo dume,
vilima kama wana-kondoo.

5 eEe bahari, ni nini kilichokufanya ukakimbia,
nawe, ee Yordani, ukarudi nyuma,
6enyi milima mkarukaruka kama kondoo dume,
enyi vilima, kama wana-kondoo?

7 fEe dunia, tetemeka mbele za Bwana,
mbele za Mungu wa Yakobo,
8 galiyegeuza mwamba kuwa dimbwi la maji,
mwamba mgumu kuwa chemchemi za maji.
Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.

Everyone uses cookies. We do too! Cookies are little bits of information stored on your computer which help us give you a better experience. You can find out more by reading the STEPBible cookie policy.