‏ Psalms 112

Baraka Za Mwenye Haki

1 aMsifuni Bwana.

Heri mtu yule amchaye Bwana,
mtu yule apendezwaye sana na amri zake.

2 bWatoto wake watakuwa wenye uwezo katika nchi,
kizazi cha watu waadilifu kitabarikiwa.
3 cNyumbani mwake kuna mali na utajiri,
haki yake hudumu milele.
4 dHata gizani nuru humzukia mtu mwadilifu,
yule mwenye rehema, huruma na haki.

5 eMema yatamjia mtu yule aliye mkarimu na mwenye kukopesha bila riba,
anayefanya mambo yake kwa haki.
6 fHakika hatatikisika kamwe,
mtu mwenye haki atakumbukwa milele.
7 gHataogopa habari mbaya,
moyo wake ni thabiti, ukimtegemea Bwana.
8 hMoyo wake ni salama, hatakuwa na hofu,
mwishoni ataona ushindi dhidi ya adui zake.
9 iAmetawanya vipawa vyake kwa ukarimu akawapa maskini;
haki yake hudumu milele;
pembe yake itatukuzwa kwa heshima.

10 jMtu mwovu ataona na kuchukizwa,
atasaga meno yake na kutoweka,
kutamani kwa mtu mwovu kutaishia patupu.
Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.