‏ Psalms 111

Sifa Za Bwana Kwa Matendo Ya Ajabu

1 aMsifuni Bwana.

Nitamtukuza Bwana kwa moyo wangu wote,
katika baraza la wanyofu na katika kusanyiko.

2 bKazi za Bwana ni kuu,
wote wanaopendezwa nazo huzitafakari.
3 cKazi zake zimejaa fahari na utukufu,
haki yake hudumu daima.
4 dAmefanya maajabu yake yakumbukwe,
Bwana ni mwenye neema na huruma.
5 eHuwapa chakula wale wanaomcha,
hulikumbuka agano lake milele.
6 fAmewaonyesha watu wake uwezo wa kazi zake,
akiwapa nchi za mataifa mengine.
7 gKazi za mikono yake ni za uaminifu na haki,
mausia yake yote ni ya kuaminika.
8 hZinadumu milele na milele,
zikifanyika kwa uaminifu na unyofu.
9 iAliwapa watu wake ukombozi,
aliamuru agano lake milele:
jina lake ni takatifu na la kuogopwa.

10 jKumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima,
wote wanaozifuata amri zake wana busara.
Sifa zake zadumu milele.
Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.

Everyone uses cookies. We do too! Cookies are little bits of information stored on your computer which help us give you a better experience. You can find out more by reading the STEPBible cookie policy.